July 15, 2015

KIKOSI CHA STAND MSIMU ULIOPITA.
Unaweza kusema  ni jeuri ya fedha kwani uongozi wa Stand United umefunguka kuwa kwa sasa unasubiri kwa hamu michuano ya Kombe la Kagame ili kupata nafasi ya kuangalia wachezaji wa kimataifa.

 Hii ni baada ya siku kadhaa klabu hiyo kuingia mkataba  wa miaka miwili na kampuni ya  Acacian ambayo inamilikiwa na migodi ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara kwa kiasi cha bilioni mbili na milioni 400.

Mwenyekiti wa timu hiyo, Aman Vincent, amefunguka kuwa wanasubiri kwa sasa michuano ya Kagame na wao kama klabu kujipanga kuangalia uwezo wa wachezaji ambao wanawahitaji katika kikosi chao.

Kiongozi huyo alisema katika usajili wao lazima wawe makini ili kuweza kufanya vyema, tofauti na msimu uliopita ambapo walikuwa ni wageni wa ligi hiyo.

“Tunataka kufanya usajili ambao utatubeba msimu ujao, lakini kwa sasa tutampa nafasi kocha na viongozi kuifanyia kazi michuano ya Kagame kuhakikisha tunasajili wachezaji wenye uwezo,” alisema Aman.


Ikumbukwe kikosi hicho kitakuwa chini ya makocha Patrick Liewig, Mganda, Martin Lule na mzalendo Athuman Bilali ‘Bilo’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic