July 17, 2015

JULIO AKIWA NA KIKOSI CHAKE CHA MWADUI BAADA YA KUTWAA UBINGWA WA LIGI DARAJA LA KWANZA.
Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ameendelea kutamba kuwa kikosi chake kitakuwa hatari msimu ujao na kudai kuwa yuko makini katika kuhakikisha anatengeneza kombinesheni ambayo itafanya vizuri hasa kwenye safu ya ushambuliaji.


Kocha huyo anatafuta kombinesheni ya Paul Nonga, Rashid Mandawa, Bakari Kigodeko na Kelvin Sabato.

Julio ambaye yupo na Mwadui kambini katika Mgodi wa Mwadui mkoani Shinyanga, amesema timu yake haichezi michezo ya kirafiki mpaka pale atakapokamilisha kutengeneza kombinesheni kwenye kikosi chake.

“Watu wanaweza kusema najisifu lakini hapa ukweli wachezaji niliosajili safari hii ni wazuri, Mwadui itakuwa tishio msimu ujao na kwa sasa katika fundisha yangu kikubwa natengeneza kombinesheni kuhakikisha wachezaji wanakuwa vizuri, hasa mbele kwenye safu ya ushambuliaji.


“Nikimalizana na hilo ndiyo nitafikiria kuanza kutafuta michezo ya kirafiki maana hapo ndiyo kikosi changu kitakuwa vizuri, kule wakikutana na Nonga inakuwa balaa,” alisema Julio.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic