July 17, 2015


Kiungo mpya wa Azam FC, Jean Baptiste Mugiraneza ‘Migi’, amepewa jezi namba 16 ambayo iliwahi kuvaliwa na Mrisho Ngassa alipokuwa klabuni hapo, lakini habari mbaya ni kuwa ameng’oka jino akiwa mazoezini.


Migi, raia wa Rwanda, amejiunga na Azam FC hivi karibuni na kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo akitokea APR ya nchini kwao.

 Migi ameiambia SALEHJEMBE kuwa hajui kama atashiriki katika michuano ya Kombe la Kagame kwa kuwa ameng’oka jino akiwa mazoezini.

Migi alijibu hivyo baada ya kuulizwa juu ya timu atakayoichezea katika michuano hiyo ya Kagame. “Nilitakiwa kuichezea Azam na siyo APR, lakini sijui kama nitacheza tena kwa kuwa nimepata tatizo kwa kung’oka jino nikiwa mazoezini leo (jana).

“Nilikuwa hospitali, jina silijui lakini ni maeneo ya Temeke, nimeambiwa natakiwa kupumzika kwa wiki moja,” alisema Migi. Alipopigiwa Daktari wa Azam FC, Mbarouk Mlinga, simu yake haikupokelewa.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic