July 24, 2015


Kufuatia presha ya shindano la kusaka vipaji la Bongo Star Search (BSS), mshiriki mwenye namba 08126 ambaye jina lake halikuweza kupatikana, alijikuta katika wakati mgumu kutokana na kupoteza fahamu baada ya majaji kumwambia hana nafasi ya kuendelea kushiriki.


Usaili wa BSS kwa Dar es Salaam ulianza juzi na unatarajiwa kufikia tamati leo Ijumaa ambapo zaidi ya washiriki 1,000 wamejitokeza katika kinyang’anyiro hicho ambapo watakaopatikana wataunganishwa na washiriki kutoka mikoa ya Mwanza, Arusha na Mbeya.
 
MAJAJI; RITA, MASTER JAY NA SALAMA.
Mshiriki aliyekutwa na majanga hayo alianguka na kuzimia baada ya Jaji Joachim Kimario ‘Master Jay’ kumtaka aondoke jukwaani kutokana na kutoimba vizuri, hali ambayo ilisababisha akimbizwe hospitali.

Mkurugenzi wa Benchmark Production, Rita Poulsen ‘Madam Rita’, amesema tukio hilo limetokea bahati mbaya na kudai kuwa wana kibarua kigumu katika kuwapata waimbaji kwa kuwa wengi waliojitokeza ni wenye vipaji vya kawaida tofauti na mikoa mingine.

“Bado tunaendelea na usaili washiriki waliojitokeza ni wengi mno kwa upande wa Dar, lakini tuna wakati mgumu kwani tumeshapitia washiriki wengi lakini hatujapata wale wa kutusisimua, labda hadi tutakapomaliza.

“Mara baada ya kuwapata tutawachuja washiriki mpaka wabaki 50, kisha tutakuwa na ‘top 20’ kisha ‘top 5’ kisha kusaka mshindi,” alisema Madam.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic