July 22, 2015


Nahodha wa Simba, Mussa Hassan Mgosi, amewatoa hofu Yanga kwa kuwaambia wasife moyo kutokana na kuanza vibaya kwenye michuano ya Kagame.


Yanga ilianza kwa kuchapwa mabao 2-1 na Gor Mahia kwenye mchezo wa kwanza wa Kombe la Kagame, lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Taifa Stars amewaambia wasijali, hayo ni matokeo ya kawaida.

Mgosi alisema katika soka kufungwa ni jambo la kawaida kabisa, ambapo aliwashauri Yanga kuangalia ni wapi walikosea katika mchezo uliopita ili kufanya vizuri kwenye michezo ijayo.
“Unajua katika soka kuna matokeo mengi, kama hivyo, kufunga, kufungwa au sare, hivyo sioni kama Yanga walifanya vibaya sana.

“Kitu ninachoweza kuwashauri ni kuangalia wapi walikosea kwenye mchezo dhidi ya Gor Mahia na kurekebisha ili waweze kufanya vizuri kwenye michezo ijayo.


“Mimi binafsi ile mechi sikuiangalia, si unajua tulikuwa kambi kwa muda mrefu na siku ile ndiyo tulirudi, hivyo sikuweza kucheki ila kwa jinsi nilivyohadithiwa, ninaamini Yanga bado wana nafasi kubwa sana ya kufanya mabadiliko na kila kitu kikaenda sawa na ikiwezekana wakatwaa ubingwa,” alisema Mgosi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic