Wakati straika wa Simba, Mrundi, Laudit
Mavugo, akitarajiwa kutua kambini visiwani hapa ndani ya siku mbili hizi,
mashabiki wa klabu hiyo juzi walijitokeza kwa wingi kwenye Uwanja wa Amaan
kuhudhuria mazoezi ya kikosi hicho wakiamini Mrundi huyo angekuwepo uwanjani
hapo.
Lakini Kocha Msaidizi wa Simba,
Selemani Matola, amethibitosha kuwa, Mavugo atatua Zanzibar ndani ya siku
mbili.
Matola amesema mbali na Mavugo, Simba
pia inawasubiri wachezaji wengine wawili, kiungo mshambuliaji Mrundi aliyemtaja
kwamba ni hatari uwanjani aliyemkumbuka kwa jina moja la Pekie na kiungo Mwinyi
Kazimoto. Mashine hizo zinasubiriwa kwenda kukamilisha kikosi kazi cha Simba
msimu ujao wa ligi kuu.
Pekie anatokea Vital’O kama ilivyo kwa
Mavugo wakati Kazimoto ameshasaini mkataba wa miaka miwili akitokea Al Markhiya
ya Qatar.
“Mwinyi atatua muda wowote kuanzia
sasa, lakini Mavugo tutampokea ndani ya siku mbili hizi, atatua pamoja na
kiungo mmoja mshambuliaji anayetoka naye timu moja, namkumbuka kwa jina moja la
Petie,” alisema Matola.








0 COMMENTS:
Post a Comment