July 21, 2015


Mashabiki wa Real Madrid wameuangushia lawama uongozi wa klabu hiyo kwamba unapenda fedha kuliko kuangalia maandalizi ya kikosi chao.


Wakati wapinzani wao Barcelona wakiwa Marekani kwenye joto, wao wamejichimbia Australia ambako kuna baridi. Mashabiki hao wamekuwa wakipinga kupitia mitandao ya kijamii, pia tovuti ya klabu hiyo.

Hali ya hewa ya Australia sasa ni nyuzi joto 5 hadi 10, jambo ambalo wanaona si sahihi kwa maadalizi ya timu.


Kwa hapa nyumbani, Simba nayo ilijichimbia mjini Lushoto kwa ajili ya maandalizi ambako hali yake ya hewa ni kama Australia.

Lakini kocha wa viungo na mtaalamu wa chakula wa Real Madrid, Miguel Ángel Duque Cano, ameliambia gazeti la MARCA kwamba hakuna tatizo kwa wao kufanya hivyo.

“Kwenye baridi kuna mambo mengi, kikubwa kabla ya mazoezi wachezaji wapashe vizuri. Lakini kwenye baridi wachezaji wanapumzika sana na hili ni jambo jema.

“Pia kufanya mazoezi kwenye baridi kunachangia misuli kujijenga vizuri, hivyo ni sahihi kabisa,” alisema.


Mashabiki hao walikuwa wanaamini Madrid imekwenda kwenye baridi lakini inachoangalia ni kujitangaza kwenye soko la Australia tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic