July 21, 2015

KATWILA (MWENYE FULANA YA NJANO) AKIZUNGUMZA NA WACHEZAJI WALIOJITOKEZA KUWANIA KUSAJILIWA NA MTIBWA SUGAR....Mtibwa Sugar imepania kupata vipaji vipya ambavyo vitajumuishwa katika kikosi chake.


Tayari imeanza kufanya kazi hiyo jijini Dar es Salaam kupitia kwa benchi lake la ufundi.

Kocha wake Mkuu, Mecky Maxime na msaidizi wake, Zuberi Katwila ndiyo wamekuwa wakiendesha zoezi hilo.

Siku chache zilizopita, zoezi hilo lilifanyika kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

“Lengo ni kuchagua vijana kadhaa wenye vipaji ambao tunaamini watakuwa msaada baada ya kukaa na sisi.

“Lakini pia tunaangalia nini cha kuongeza katika kikosi chetu kulingana na mahitaji yetu,” alisema Maxime.

Mtibwa Sugar ni kati ya timu chache ambazo huwainua wachezaji wasiokuwa na majina, au huwapa nafasi wachezaji wanaoonekana wakongwe na wameisha hadi wanapoibuka na kuwa lulu tena.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic