July 29, 2015


Kiungo wa Simba, Jonas Mkude, hali yake ni tete baada ya kupata maumivu ya goti yaliyomuweka nje ya uwanja tangu Jumamosi iliyopita.


Mkude yuko pamoja na kikosi cha Simba visiwani hapa wakijiwinda vikali kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara lakini yeye tangu Jumamosi amekuwa hafanyi mazoezi magumu kutokana na maumivu hayo.

SALEHJEMBE lilishuhudia Mkude akiwa nje ya uwanja wakati timu hiyo ikifanya mazoezi magumu na aliingia dimbani kufanya mazoezi mepesi tu.

Imeelezwa kuwa ugumu wa mazoezi ya viungo yanayoongozwa na kocha wa viungo wa timu hiyo, Dusan Momcilovic, ndiyo yanayochangia wachezaji wengi kuumia.
“Kweli mazoezi ni magumu mno, kila siku tunalala hoi,” alisema mchezaji mmoja wa timu hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina.

Daktari wa Simba, Yassin Gembe, ameliambia gazeti hili kuwa maendeleo ya Mkude ni mazuri na atarejea uwanjani hivi karibuni.


“Siwezi kusema atarejea lini lakini ni hivi karibuni ndiyo atakuwa fiti kabisa,” alisema Gembe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic