July 18, 2015

Mshambuliaji mpya wa Yanga, Donald Ngoma amelambwa kadi nyekundu.
Ngoma amepigwa kadi hiyo baada ya kumsukuma beki wa Gor Mahia ambaye alipanda kwenye mguu wake katika dakika ya 24 ya mchezo.


Mechi hiyo ya ufunguzi wa michuano ya Kombe la Kagame inaendelea sasa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo lilionyesha kumuudhi Ngoma raia wa Zimbabwe aliyekuwa na kadi ya njano tayari, akamsukuma na mwamuzi akampa kadi nyingine ya njano na kuwa nyekundu.

Ngoma alijikuta akiangua kilio baada ya kutolewa nje . Hadi sasa Yanga ina bao moja kama ilivyo kwa Gor Mahia ambayo ilisawazisha katika dakika ya 24 kupitia Shakava.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic