July 15, 2015



Beki wa kulia wa Yanga, raia wa Ghana, Joseph Zuttah, ameanza kuyaona maisha yake katika klabu hiyo kuwa magumu baada ya kudai kuwa ana kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha anapata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

Zuttah amejiunga na Yanga hivi karibuni akitokea Klabu ya Medeama ya Ghana na kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia timu hiyo ambayo kwa sasa inajiandaa na Michuano ya Kagame inayoanza kutimua vumbi Jumamosi hii hapa nchini.

 “Kusema kweli bado sina uhakika wa kupata nafasi katika kikosi cha kwanza ila anayejua hilo ni kocha.


“Nasema hivyo kwa sababu nafasi ninazocheza uwanjani zote zina wachezaji mahiri na wenye uwezo mkubwa, kwa mfano Juma Abdul, Salum Telela, Mbuyu Twitte na Simon Msuva, wote ni wazuri, hivyo kocha ndiye anayejua kama nastahili kuwepo katika kikosi chake cha kwanza,” alisema Zuttah.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic