Runinga
ya Azam TV leo rasmi imezindua uonyeshwaji wa Ligi maarufu ya Hispania ya La
Liga.
Uzinduzi
huo umefanyika makao makuu ya Azam TV, Tabata jijini Dar es Salaam na wageni
kadhaa walialikwa.
Kupitia
ving’amuzi vya Azam TV, sasa watu wataweza kuona mechi mbalimbali za La Liga
wakianza na ile ya Ijumaa ijayo kati ya Malaga dhidi ya Sevilla.
Azam TV
inakuwa kampuni ya kwanza ya Tanzania inayomiliki runinga kupewa haki ya
kuonyesha mechi za La Liga ambayo ni ligi yenye mafanikio makubwa zaidi katika
kipindi hiki.
...TORRINGTON AKIFANYA YAKE. |
TIDO MHANDO AKIFAFANUA JAMBO... |
SEHEMU YA WAGENI WAALIKWA, SHAFFIH DAUDA, SAID TULLY NA EDO KUMWEMBE WALIKUWEPO. |
FLORIAN KAIJAGE ALIYEKUWA MWENDESHA SHUGHULI PIA ALIKUWEPO. |
0 COMMENTS:
Post a Comment