Runinga
ya Azam TV leo inazindua rasmi kuhusiana na uonyesha wa Ligi maarufu ya
Hispania ya La Liga.
Leo
ndiyo unafanyika uzinduzi rasmi baada ya Azam TV kukabidhiwa haki za kuonyesha
La Liga ambayo ndiyo ligi inaonekana kuwa na mafanikio makubwa zaidi katika
kipindi cha miaka mitano sasa.
Mfano msimu
huu, La Liga ndiyo imetoa wanamichezo bora wa dunia mfululizo kuliko nyingine
yoyote. Pia sasa mabingwa wote wa Ulaya wanatokea La Liga.
Hivyo
wenye ving’amuzi vya Azam TV watapata nafasi ya kushuhudia moja kwa moja, pia
marudio ya mechi hizo za La Liga.
0 COMMENTS:
Post a Comment