August 2, 2015


Hawa ndiyo mabingwa wapya wa Kombe la Kagame.

Wanaitwa Azam FC.


Azam FC iumeifunga Gor Mahia kwa mabao 2-0 na kubeba ubingwa wa Kagame wakiwa hawajafungwa hata bao moja.

Mwaka 2002, Tusker ya Kenya ilifanya hivyo, lakini Azam FC imefanya hivyo huku ikiwa haijafungwa hata bao moja, Simba na Yanga hazijawahi kufanya hivyo.

Bao la kwanza la Azam FC lilifungwa na John Bocco ambaye aliipangua beki ya Gor kabla ya kupiga krosi safi kabisa iliyomfikia Bocco akamaliza kazi.

Bao la pili, likafungwa Kipre ambaye alipiga mpira wa adhabu na kipa wa Gor akadhani unatoka.


Baada ya hapo, Gor iliendelea kupambana lakini ilishindwa kuukamata mziki wa Azam FC ambao walikuwa safi huku beki Serge Wawa akimtuliza mshambuliaji hatari Michael Olunga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic