Na
Saleh Ally
BAADA
ya mechi 26 za Ligi Kuu Bara msimu uliopita, Yanga ndiyo walitangazwa kuwa mabingwa
rasmi. Hata hivyo, mechi tatu kabla walishajua kuhusiana na cheo chao hicho cha
Wafalme Wapya.
Hadi
mwisho kabisa wa ligi, Yanga walikuwa wameshinda mechi 17 kati ya 26
walizocheza na kuwa timu iliyoshinda mechi nyingi zaidi kwani Azam FC iliyokuwa
ya pili na Simba katika nafasi ya tatu, kila moja ilikuwa imeshinda mechi 13
tu.
Ukiachana
na ushindi huo ambao ulionyesha Yanga ilikuwa na kikosi imara, safu yake ya
ulinzi ilifungwa mabao 18, sawa kabisa na safu ya ulinzi ya Azam FC, huku Simba
katika nafasi ya tatu ikiruhusu mabao 19.
Nafasi
ya nne Mbeya City iliruhusu mabao 22 na katika nafasi ya tano, Coastal Union
ikaruhusu mabao 25.
Kwa
upande wa mabao ya kufunga, Yanga pia iliongoza ikiwa na 52, ikifuatiwa na
Simba iliyofunga 38 na kuipita Azam FC katika nafasi ya pili ikiwa na mabao 36.
Mbeya City ilimaliza na mabao 22 na Coastal Union 21.
Utaona
kitu hapo, licha ya kuwa na tofauti kubwa kati ya Yanga na timu nyingine katika
ushindi wa mechi na mabao ya kufunga, hakuna tofauti kubwa katika mabao ya
kufungwa.
Mabao
ya kufungwa ndiyo jibu la ubora wa safu ya ulinzi ya timu husika. Kweli Yanga
imekuwa na safu nzuri ya ulinzi, inayolingana na mshindi wa pili, lakini yenye
tofauti ya bao moja tu na mshindi wa tatu ambaye ni Simba.
Kama
utazungumzia ubora wa juu katika msimu kwa maana ya uchambuzi wa kikosi kwa
eneo, safu ya ushambulizi ya Yanga ndiyo ilikuwa bora zaidi kwa msimu huo na
hilo halina ubishi.
Lakini
kama ni safu ya ulinzi, Yanga inakuwa si bora zaidi lakini ni moja ya bora.
Maana iko sawa na Azam FC, pia ina tofauti ya bao moja zaidi la kufungwa na
Simba iliyokuwa nafasi ya tatu.
Utaona
safu ya ulinzi ya Simba iliyokuwa inaongozwa na vijana kama Juuko Murshid na
Hassan Khatibu ilivyoweza kupambana na kuwa anga za safu ya ulinzi inayoongozwa
na wachezaji wakongwe na tegemeo kwa taifa kama Kelvin Yondani na Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Kwa
maana ya takwimu, kuna tofauti kubwa kati ya safu ya ushambuliaji ya Yanga
msimu uliopita na ile ya Simba na vikosi vingine. Lakini hakuna tofauti kubwa
kati ya safu hiyo ya ulinzi ya Yanga na Simba.
Usisahau
safu ya ulinzi ya Yanga inaongozwa na mabeki wawili wakongwe na tegemeo kwa
taifa letu, awa ni Cannavaro na Yondani.
Binafsi
ninaamini safu hiyo ilipaswa ifanye vizuri zaidi na huenda ndiyo chanzo cha
kuona imeshindwa kufanya vyema katika mechi za majaribio na sasa uongozi wa
Yanga umeamua kuiongezea nguvu katika safu ya ulinzi.
Ajabu
ukiwasikia watu wengi wanazungumzia matatizo ya ulinzi, zaidi wanasema
kuhusiana na Yondani kwamba ameisha!
Hakuna
anayeeleza Yondani ameisha vipi, lakini kitakwimu inaonyesha wazi ambaye
kiwango chake kimeshuka ni nahodha Cannavaro. Huenda suala la heshima
limetangulia na inakuwa vigumu kumueleza ukweli nahodha huyo wa Yanga na Taifa
Stars.
Cannavaro
ni msikivu, mnyenyekevu, mtu mzuri na mwenye nidhamu. Lakini uchezaji wake
unaonyesha wazi kuwa hayuko vizuri kama ilivyokuwa misimu miwili iliyopita.
Mbaya
zaidi, haelezwi ukweli ikionekana si sahihi kumueleza nahodha na hilo ni kosa
kubwa kwa kuwa inazidi kumdidimiza.
Niliwahi
kumhesabia Cannavaro, karibu msimu mzima katika mechi zilizochezwa Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam, mipira yote 56 ya vichwa dhidi ya washambuliaji
alipiga yeye isipokuwa miwili tu dhidi ya Felix Sunzu.
Wakati
Taifa Stars ilipocheza mechi ya kirafiki na kufungwa bao 1-0 na Ivory Coast,
Didier Drogba aliruka mara saba juu na Cannavaro. Tembo huyo alipiga vichwa
viwili na kimoja akafunga bao lakini vitano vyote alipiga beki huyo.
Lakini
hivi karibuni imekuwa kawaida tu kwa washambuliaji kupiga mipira ya vichwa
mbele ya Cannavaro na uliona Michael Olunga wa Gor Mahia alivyofanya.
Suala
la kujipanga na kuipanga safu yake ya ulinzi limekuwa tatizo kwa Cannavaro
ambaye alikuwa na uwezo mkubwa na ndiyo moja ya sifa za juu za ‘kitasa’ au
namba tano. Sasa safu yake ya ulinzi inapotea njia tu na haya matatizo si ya Yondani,
ni yake Cannavaro.
Yanga
imefanikiwa kuimarisha kiungo cha ulinzi kwa kumsajili, Thabani Kamusoko kutoka
Zimbabwe, hili ni sahihi na awali nililieza.
Pamoja
na kumsajili Vicent Bossou kutoka Mali kuimarisha ulinzi, kama Yondani atabaki
nje, basi Cannavaro lazima arekebishe hayo, la sivyo itakuwa kazi bure katika
safu ya ulinzi na huenda hakutakuwa na maana ya mabadiliko hayo.
Kingine
nisisitize, suala la ukimya kwa maana ya heshima au kuoneana haya, halijengi.
Tuache unafiki ili tuelezane ukweli kwa faida ya soka ya Tanzania.
0 COMMENTS:
Post a Comment