Kiungo mkabaji mpya wa Azam FC, Mnyarwanda, Jean Baptiste
Mugiraneza ‘Migi’ ametamka kuwa hataki kutoka kwenye kikosi cha kwanza cha
Muingereza, Stewart Hall kinachojiandaa na Ligi Kuu Bara.
Migi alipata ujasiri wa kuongea kauli hiyo baada ya kucheza mechi
zote za Kagame akicheza namba sita inayochezwa na Muivory Coast, Kipre Balou na
Mudathiri Yahaya.
Kiungo huyo anayetumia mguu wa kushoto, alitua nchini hivi
karibuni akisaini mkataba wa miaka miwili.
Migi alisema kuwa kikubwa amejipanga kupambana ili kuhakikisha
anaendelea kuwepo kwenye kikosi cha kwanza.
Migi alisema, upo ushindani mkubwa wa namba kwenye timu hiyo,
hivyo pale mchezaji unapopata nafasi ya kucheza ni lazima ucheze kwa kujituma
ili kocha akuamini aendelee kukupanga kikosini.
“Nisingependa kuwazungumzia
sana wachezaji ninaocheza nao nafasi moja uwanjani, lakini kwa kifupi tu, mimi
nimepanga kuendelea kuwepo kwenye kikosi labda litokee tatizo la majeruhi pekee
lakini siyo uwezo.
“Kikubwa ninashukuru kupewa nafasi ya kuaminika kwenye timu na
kuingizwa kwenye kikosi cha kwanza moja kwa moja mara baada ya kujiunga na Azam
tukishiriki Kombe la Kagame,” alisema Migi anayeichezea timu ya taifa ya Rwanda
‘Amavubi’.
0 COMMENTS:
Post a Comment