August 15, 2015


Kesho Jumapili Yanga inacheza mechi ya kirafiki na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya katika kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katika kikosi cha Yanga, yumo kiungo mshambuliaji Deus Kaseke aliyesajiliwa hivi karibuni kutoka Mbeya City, ambaye angeweza kuutumia mchezo huo kuwaaga wachezaji wenzake.

Pengine Kaseke angecheza kipindi cha kwanza akiwa Mbeya City kisha kipindi cha pili akacheza Yanga kama alivyofanya Geoffrey Mwashiuya pindi timu yake ya zamani ya Kimondo ilipocheza na mabingwa hao watetezi wa ligi kuu.

Kaseke amesema kuwa, haoni sababu ya kuichezea Mbeya City kwani tayari yeye ni mchezaji wa Yanga na hawezi kuichezea timu nyingine.

“Nicheze Mbeya City? Hapana, nitacheza Yanga kwa dakika zote tena kwa kiwango changu kilekile, watu wasitarajie kwamba nitazitumikia timu zote kwa vipindi tofauti. Waelewe tu kuwa mimi ni mchezaji wa Yanga.

“Wachezaji wengi hasa wa kimataifa wamekuwa wakifanya hivyo, lakini kwangu sijafikiria,” alisema Kaseke ambaye amejihakikishia namba kwenye kikosi cha Yanga.

Akizungumzia mchezo huo, Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi, alisema: “Nilikuwa Dar es Salaam, ndiyo narudi Mbeya sasa (jana), nitaiandaa timu kesho (leo Jumamosi) kwa mechi hiyo.”


Katika mchezo huo, Yanga inatarajiwa kuwatumia nyota wake wengine wapya akiwemo Donald Ngoma, Thabani Kamusoko, Malimi Busungu, Simon Matheo, Benedict Tinocco na Haji Mwinyi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic