August 15, 2015


Yanga ipo kambini jijini Mbeya kwenye baridi kali lakini kocha wa timu hiyo, Hans van Der Pluijm anaamini hali hiyo ya hewa itawaweka fiti wachezaji wake kuweza kufanya vizuri katika mechi zao zijazo ikiwemo dhidi ya Azam FC.

Agosti 22, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Yanga itacheza na Azam mechi ya Ngao ya Jamii ambayo hukutanisha timu bingwa wa msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara na iliyoshika nafasi ya pili.
Yanga ambayo ni bingwa mtetezi ipo kambini Mbeya ambako kesho Jumapili itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine ili kujipima nguvu.

Pluijm, amesema: “Licha ya kuwepo baridi, naamini hiyo ni njia mojawapo ya kuwajenga wachezaji wangu huku tukihakikisha tunapunguza makosa yanayojitokeza mara kwa mara kwenye kikosini chetu.”

Tayari Yanga imecheza mechi mbili za kirafiki ikiwa Nyanda za Juu, Kusini na kushinda zote ikianza kwa kuitandika Kimondo kwa mabao 4-1 kabla ya kuituliza Prisons kwa mabao 2-0.

Imebakiza mechi moja dhidi ya Mbeya City ambayo ndiyo timu ngumu zaidi katika ukanda huo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic