Kiungo Justice Majabvi, amesaini mkataba wa
kuichezea Simba na amepiga mkwara mzito kwa viungo wenzake akiwemo Jonas Mkude
kuwa wajipange la sivyo watakaa benchi.
Awali, baadhi ya viongozi wa Simba hawakutaka
kabisa Majabvi asajiliwe kwa maelezo kuwa kiwango chake ni cha kawaida wakati wapo
wazawa kama Mkude, Said Ndemla, Awadh Juma na Abdi Banda wanaoweza kucheza
nafasi yake.
Lakini Kocha Dylan Kerr akawaambia viongozi
hao: “Mimi ndiye bosi na lazima mumsajili Majabvi.” Kweli Majabvi raia wa
Zimbabwe akasaini mkataba wa miaka miwili na sasa ni mali ya Simba.
Muda mfupi baada ya kusaini mkataba huo,
Majabvi akasisitiza: “Najipanga kikamilifu kucheza kikosi cha
kwanza, nimekuta watu wanacheza hapa nami nitapambana ili nicheze, naamini
hakuna linaloshindikana.
“Kwa upande wangu ninajipanga kikamilifu
kuhakikisha napigana na kuonyesha uwezo wangu wa hali ya juu ambao utamshawishi
kocha anipange katika kikosi cha kwanza na kuwapokonya namba hawa niliowakuta,”
alisema Majabvi ambaye amewahi kuichezea timu ya Vicem Hai Phong ya Vietnam.
0 COMMENTS:
Post a Comment