Na
Saleh Ally
MALAGA
ndiyo timu ya kwanza katika msimu mpya wa La Liga wa 2015-16 kucheza mechi yake
ya kwanza ya ligi hiyo nyumbani.
Mji
wa Malaga unaosifiwa kuwa na mandhari bora kabisa katika miji mingi ya Ulaya
itakuwa na ugeni wa wababe Sevilla ambao wameonyesha uwezo mkubwa katika misimu
miwili iliyopita.
Licha
ya kumkosa Carlos Bacca, Sevilla imeweza kuisumbua kwa kiwango cha juu Barcelona
ambayo ilibeba Kombe la Super Cup ya Uefa, siku kadhaa zilizopita kwa mabao 4-3.
Uwezo
waliouonyesha, sasa wanaurudisha La Liga ambako wanakutana na Malaga kwenye
Uwanja wao wa nyumbani wa La Rosaleda.
Kitu
kizuri mashabiki wa soka kuanzia Tanzania, Uganda, Rwanda na sehemu nyingine za
Ukanda wa Afrika Mashariki watapata nafasi ya kuona mechi hiyo moja kwa moja
kupitia Azam TV.
Malaga
na Sevilla zimekuwa na ushindani wa juu kabisa katika La Liga pia Copa del Rey,
ni timu ambazo kila zinapokutana, kunakuwa na mashabiki wengi na mechi yao ya
ufunguzi wa ligi, tiketi zake ziliuzwa haraka mno ndiyo maana unaweza kusema
uhakika wa Dimba la La Rosaleda linalochukua watu 30,044 kujaa pomoni, hauna
mjadala.
Malaga
imejiimarisha vilivyo na mmiliki wake Sheikh Abdullah Al Thani amekubali kutoa
fedha za kutosha ili kuhakikisha msimu ujao wanafanya makubwa zaidi.
Tayari
timu hizo zimekutana mara 30 katika michuano mbalimbali ikiwemo La Liga na Copa
del Rey na inaonekana zimekuwa na ushindani wa juu kabisa.
Sevilla
imeshinda mara 11 wakati Malaga imeshinda mara 12 na zimetoka sare 7, huku
wastani wa mabao yao ya kufunga na kufungwa ukiwa sawa kabisa.
Inawezekana
pamoja na kutaka pointi tatu muhimu ili waanze La Liga vizuri lakini Sevilla
watakuwa na hamu ya kusawazisha ili nao wawe wameshinda mara 12 na si kupoteza
mara 13.
Kasi
ya timu hizo inakupa picha kwamba hata kama hazikutani Barcelona na Madrid
lakini mechi itakuwa ngumu kwa kuwa angalia ubora wa Sevilla na ilivyoisumbua
Barcelona, lakini inapokutana na Malaga kazi inakuwa pevu kwake.
Aina
ya uchezaji wa timu zote kama unafanana kwa kiasi kikubwa kwa kuwa kweli
zinacheza Spanish Football lakini zinatumia nguvu kama ile aina ya Real Madrid.
Pasi
nyingi, kasi na krosi fupi ambazo zinaingia ndani ya boksi kutoka pembeni na
katikati, hivyo kufanya mpira uwe na ladha zaidi ya kutazama kutokana na mvuto.
Sifa
nyingine ya mechi hiyo, huenda kwa kuwa timu zote zinatumia nguvu sana,
kumekuwa na rekodi ya kadi nyekundu nyingi. Mfano katika mechi 18 zilizopita
kuanzia msimu wa 2005-06, kuna kadi nyekundu tisa zilipatikana, hata mechi ya
mzunguko wa pili wa La Liga, Malaga ikiwa nyumbani, mchezaji wake alilambwa
kadi nyekundu.
Inachoweza
kujivunia Sevilla ni hivi, kwamba katika La Liga, msimu uliopita ulikuwa wake. Ilianza
kushinda bao 2-0 katika mechi yake ya nyumbani lakini iliposafiri kwenda
ugenini ikashinda kwa mabao 3-2.
Sasa
unapozungumzia suala la ushindi kwenye Uwanja wa La Rosaleda, wageni Sevilla
ndiyo wa mwisho kushinda hapo. Je, wataendelea msimu ya msimu uliopita au
wenyeji watakomaa?
Hii
inaonyesha kiasi gani ushindani mkubwa na unavyozidi kupanda juu dhidi ya timu
hizi unavyoongeza joto katika mechi ya kesho.
Usisahau
kitu kimoja, mara baada ya La Liga kumalizika msimu uliopita, kila timu ikiwa
imecheza mechi zake 38 kwa timu zote 20, Sevilla ilikwama katika nafasi ya 5
ikiwa na pointi 76 huku Malaga ikiishia katika nafasi ya 9 ikiwa na pointi 50
tu.
Kwa
leo kutakuwa na mechi hiyo moja tu inayofungua pazia la La Liga lakini kesho
mechi nyingine nne, uhondo unaendelea ndani ya Azam TV.
0 COMMENTS:
Post a Comment