August 19, 2015


Na Aidan Mlimila
Mwishoni mwa miaka ya 80 na mwanzoni mwa miaka ya 2000 ulipokuwa ukitaja Liverpool Fc basi ulikuwa unataja timu yenye mafanikio kuliko timu nyingine yeyote katika soka la Uingereza ukiachilia mbali mafanikio waliyokuwa wameyapata kwenye soka la ulaya kwa ujumla kwa maana ya mashindano yanayoandaliwa na chama cha soka cha ulaya Uefa.

Kwa upande mwingine Liverpool ilikuwa ndiyo timu ambayo ilikuwa imetwaa mataji mengi ya ligi kuu ya Uingereza kabla rekodi yao haijavunjwa na mahasimu wao wakubwa katika soka la Uingereza klabu ya Manchester United ambayo imetwaa mataji 20 mpaka sasa mataji mawili zaidi ya Liverpool.

Ni muda mrefu sasa Liverpool imekuwa haifanyi vizuri kwenye ligi kuu ya Uingereza siyo kutwaa Ubingwa tu, bali hata uhakika wa kumaliza ndani ya timu nne za juu katika ligi kuu ya Uingereza limekuwa ni tatizo sana kwao kwa misimu mingi ya karibuni.

Tangu Brendan Rodgers alipoteuliwa kuifundisha Liverpool mwaka 2012 akitokea klabu ya Swansea moja ya kitu ambacho amefanikiwa kwa kiasi fulani ni kuiwezesha Liverpool kumaliza ndani ya timu nne za juu msimu wa 2013/14 kitu ambacho watu wa Liverpool walikuwa wamekimisi  kwa muda na ilibakia kidogo msimu huo watwae ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza kama isingekuwa makosa ambayo waliyafanya na kupelekea kukosa ubingwa dakika za mwisho.

Kabla ligi haijaanza Liverpool ilikuwa ni timu ambayo sikuipa nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri  msimu huu. Lakini baada ya mechi hizi mbili taratibu naona wameanza kunishawishi na kunifanya nianze kubadili mtazamo wangu juu yao. Ingawa ni mapema sana kuzungumzia nafasi ya timu kwa kutumia mechi mbili tu kati ya mechi 38 ambazo kila timu inatakiwa kucheza msimu mzima.

Lakini ndani ya mechi hizi mbili ambazo Liverpool wameshacheza mpaka sasa kuna kitu nimekiona ambacho nadhani kama wataendelea na mwendelezo huu basi wanaweza kuwa ndo ambayo itawashangaza wengi mwisho wa msimu (Surprise of the Season).

Kwenye idara ya ulinzi Liverpool mpaka sasa ndani ya dakika 180 hawajaruhusu nyavu zao kuguswa. Na kama inavyojulikana ili timu iweze kufanya vizuri katika ligi lazma kwanza kabisa iwe na defense imara kitu ambacho Liverpool wameweza kukionesha ndani ya mechi hizi mbili. Ingawa mtu mwingine anaweza kuhoji ubora wa timu ambazo Liverpool imekutana nazo mpaka sasa lakini binafsi wameweza kunishawishi.

Kitu kingine ambacho kinanifanya nianze kuipa nafasi Liverpool ni kuanza vibaya kwa timu ambazo zilionekana kutishia nafasi yao katika nafasi nne za juu (Top Four). Arsenal na Chelsea zimeonekana kutokuwa na mwanzo mzuri mpaka sasa Chelsea wako nyuma ya Liverpool kwa point tano huku Arsenal wakiwa nyuma kwa point tatu hii ni faida kubwa sana kwao kwa sababu kadri ambavyo wapinzani wao wanavyozidi kupata matokeo mabaya ndivyo ambavyo nafasi yao ya kufanya vizuri inapozidi kuongezeka.

Lakini pia ingizo la wachezaji kama Klyne, Benteke, na Firminio kwa kiasi kikubwa umeongeza kitu kwenye kikosi cha majogoo hao wa Merseyside. Unapokuwa na mtu kama Benteke kwenye eneo la ushambuliaji hii ina maana una mtu ambaye ana uwezo wa kukupa siyo pungufu ya magoli 20 kwa msimu na hii ni kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao wa kufunga magoli lakini pia kucheza na watu kama Courtinho na Firminio ambao wana uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi za magoli kitu ambacho kitakuwa faida kwa Benteke kumfanya afunge magoli mengi ambayo mwisho wa siku yataisadia Liverpool kukusanya point za kutosha.

Ujio wa Nathaniel Clyne pia umeongeza kitu kikubwa sana kwenye safu ya ulinzi ya Liverpool. Uwezo wake mkubwa aliokuwa nao wa kukaba pale ambapo timu inashambuliwa na uwezo wa kusukuma mashambulizi pale ambapo timu inapokuwa inashambulia bila shaka utakuwa msaada mkubwa sana kwao. 

Kitu kingine ambacho Klyne ataongeza ni uwezo wake mkubwa wa kupiga krosi kitu ambacho kitaipa Liverpool option nyingine ya kutengeneza nafasi kupitia kwenye flanks kitu kitakachokuwa faida kubwa pia kwa Christian Benteke ambaye pia ni mzuri sana hewani (aerial balls).
Na hapo ndipo Liverpool wanapoanza kunishawishi na kuanza kubadili mtazamo wangu juu yao

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic