MECHI
ya Ngao ya Jamii kati ya mabingwa watetezi wa Tanzania, Yanga na waliokuwa
washindi wa pili, Azam FC ilikuwa na burudani na mvuto kwa maana ya soka la
ushindani.
Utaona
soka lilivyokuwa likichezwa, kila upande ulionekana umepania kushinda ndani ya
dakika 90 na suala la kupoteza muda lilipata asilimia chake sana.
Mwishoni
kabisa wakati inaonekana kila timu ilianza kujenga hisia za kujilinda na
ikiwezekana bora kwenda kwenye penalti kwa kuwa kila upande ulionekana ni
mgumu.
Angalau
utaona, hata ule ugonjwa wa kutokuwa na wachezaji wanaopiga mashuti kwenye Ligi
Kuu Bara kwa misimu mitatu au minne sasa, unaonekana unaanza kupona.
Kwani
upande wa Yanga walijaribu zaidi ya mara nne, hali kadhali Azam FC walifanya
hivyo na kuonyesha ili ni mechi kila timu inataka kushinda.
Hisia
za kwamba ushindani wa ligi sasa unahamia kwa Azam na Yanga, unaweza ukawa
unajengeka kutokana na timu hizo zilivyovutana na kucheza soka la ushinda kwa
asilimia kubwa sana.
Niwe
wazi, ilikuwa ni mechi nzuri ambayo inaweza ikaingizwa kwenye tafsiri nyingi
kupitia mpira wetu ikiwemo ile ya kama timu zitaendelea kucheza kwa kiwango
hicho kwa msimu wote, dalili za mpira wa Tanzania kupanda, zitakuwa wazi.
Tofauti
kubwa ambayo niliiona, wachezaji wengi walishindwa kuwa wazi au huru.
Hawakujiachia na kuonyesha vipaji vyao kwa uwezo ulio sahihi au ule walionao.
Wengi
walifuata mafunzo ya walimu, walihakikisha wanatekeleza kile ambacho mwalimu
anataka, lakini si nyongeza kubwa kutokana na uwezo walionao au majaaliwa ya
vipaji walivyonavyo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Katika
mechi hiyo pamoja na kuvutia kweli, bado ilionekana mechi hiyo haikuwa na mtu
ambaye alikuwa ana uwezo wa kubadili mechi peke yake, iwe ni upande wa Yanga au
Azam FC.
Angalau
Kipre Tchetche alijaribu, mara kadhaa alijaribu kuonyesha tofauti, lakini si
kwa kiwango cha kusema alikuwa “the game killer”, yaani mtu anayeweza kumaliza
mchezo.
Mtu
anayeweza kumaliza mchezo kwanza kabisa lazima acheze ndani ya mfumo wa
mwalimu, lakini awe na ziada ambayo hata mwalimu au mashabiki hawakutegemea
inaweza kutokea au anaweza kufanya.
Si
lazima afunge; kuna mambo matatu anaweza kuafanya. Kwanza akawa ndiye
anaanzisha mashambulizi kwa kushikilia moyo wa timu, akachezesha na
kuwachanganya wapinzani huku ikionekana yeye ndiye tatizo na ameshindikana.
Anaweza
kuwa ndiye hatari kwa maana ya kupiga krosi safi, anaweza kuwa mtu anayepiga
vizuri mipira ‘iliyokufa’, kama timu moja wakipata afaulo basi unajua game
imeisha kwa asilimia 90.
Tatu,
mfungaji. Mmaliziaji bora ambaye akiingia ndani ya boksi, timu pinzani
wanafumba macho kwa kuwa kusalimika kwao kunakuwa ni asilimia 10 tu.
Najua
hauwezi kupinga enzi zile za kina Zamoyoni Mogella, Edibily Lunyamila, marehemu
Hamis Thobias Gaga au wakongwe kama akina Sunday Manara. Swali, sasa hatuna
wachezaji wa aina yao?
Ladha
ya mpira haimaliziki kupitia ndani ya mfumo pekee ambao kisoka inaonekana ni
ubongo wa kocha. Sasa ubongo wa mchezaji nao una nafasi yake na lazima ufanye
kazi ili kutengeneza kikosi kilicho bora chenye uhakika na matokeo bora.
Kama
mabingwa na washindi wa pili wanaonyesha hawana hata mchezaji mmoja anaweza
kuwa na uwezo wa kubadili matokeo hasa mifumo ya makocha inapokwama, basi
tatizo ni kubwa.
Bado
Azam FC na mabingwa Yanga wanaweza kuwa taswira ya ligi yetu ya Bara. Hivyo ni
lazima wachezaji sasa wajitambue na wacheze kwa uwezo wao walionao ikiwezekana
kuuongeza kwa juhudi.








0 COMMENTS:
Post a Comment