August 24, 2015

NIANG ALIPOWASILI DAR

Mshambuliaji Papa Niang ametamba kwamba atafuzu majaribio Simba bila ya hofu.



Niang ametua nchini kwa ajili ya kufanya majaribio na leo ataichezea Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati inaivaa Mwadui FC katika mechi ya kirafiki.

Niang amesema ana uhakika wa kufanya vizuri licha ya kwamba hakuwa na mazoezi ya kutosha.

"Kweli nilipumzika muda kidogo, lakini ninaamini uwezo wangu. Kwa mazoezi ya siku chache na mechi moja nitakayocheza, hakuna kitakachonizuia.

"Kuzungumza kuhusu mwenyewe si jambo jema, huenda itakuwa vizuri watu wakaniona nikiwa kazini,"alijitapa.

Msenegali huyo inaelezwa ni mdogo wa Papa Niang, mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya Senegal, Mamadou Niang.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic