August 12, 2015


Straika nyota wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe, amemuangalia beki kisiki wa Azam FC, Muivory Coast, Pascal Wawa na kutamba kuwa lazima aipenye safu ya ulinzi ya timu hiyo baada ya kuzisoma mbinu za wapinzani wao.


Yanga ikiwatumia washambuliaji wake Donald Ngoma, Malimi Busungu, ilishindwa kupenya kwenye safu ya ulinzi ya Azam FC inayoongozwa na Wawa, Aggrey Morris, Shomari Kapombe na Said Morad kufunga bao kwenye mechi ya robo fainali ya Kombe la Kagame iliyomalizika kwa Yanga kutolewa kwa penalti 5-3.

Timu hizo zinatarajiwa kukutana kwa mara nyingine kwenye mechi ya Ngao ya Jamii itakayochezwa Agosti 22, mwaka huu Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Tambwe ameiambia SALEHJEMBE kuwa amegundua udhaifu wa mabeki wa timu hiyo ambao ni wazito, hivyo hawana kasi ya kushindana na mawinga wao Simon Msuva, Geofrey Mwashiuya, Andrey Coutinho na Deus Kaseke.

Aliongeza kuwa, hata mabao yao wanataka yatokee pembeni wakiwatumia mawinga kwa kupiga krosi safi kabla ya kufunga baada ya kuona katikati kugumu kupita kwenye ukuta huo.

“Kwenye mechi na Azam ile ya robo fainali ya Kagame waliyotutoa kwa penalti, nikwambie ukweli tu kama angeanza Msuva ninaamini lazima tungewafunga.

“Hiyo ni baada ya kuujua mfumo wao wa kujaza mabeki wengi katikati, hivyo tumepanga kutumia mawinga tukitokea pembeni kulishambulia goli lao na siyo katikati.


“Tumeuona udhaifu wa mabeki wao, wengi wao ni wazito, akiwemo Wawa ambaye hana kasi ya kukimbia, hivyo tukiwatumia mawinga wetu akina Msuva na Mwashiuya kuwambiza, ninaamini lazima tutawafunga,” alisema Tambwe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic