August 24, 2015

  
Na Saleh Ally, Istanbul
Wachezaji wa Taifa Stars wamepata nafasi ya kuuona uwanja unaomilikiwa na klabu kongwe na maarufu ya hapa Uturuki ya Galatasaray, huku wengi wakionekana kufurahia.


Galatasaray inajulikana kutokana na ubora wake pia historia au rekodi nzuri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
 

Wachezaji wa Stars wakiwa njiani kutoka jijini Istanbul kwenda katika mji mdogo wa Kartepe walipita karibu na Uwanja wa Turk Telecom Arena ambao unamilikiwa na Galatasaray.

Kikosi cha Taifa Stars kimewasili nchini Uturuki tayari kwa kambi ya wiki moja kujiandaa kuivaa Nigeria.

Baada ya kuwasili Istanbul ilianza safari hadi kwenye mji wa Kartepe ulio juu ya milima kabisa ambako wataweka kambi yao katika Hoteli kubwa ya kitali ya The Green Park.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic