August 23, 2015


Kiungo Mkenya, Victor Wanyama amesema anataka kuondoka katika kikosi cha Southampton.


Wanyama ameuambia uongozi wa Southampton inayoshiriki Ligi Kuu England kwamba anataka kuondoka katika klabu hiyo.

Sababu ya msingi aliyoitoa ni kwamba hana raha klabu hapo, angependa kutafuta au kuendeleza maisha yake ya soka sehemu nyingine.



Habari hiyo imeonyesha kuushitua uongozi wa klabu hiyo ambayo inamtegemea kama kiungo namba moja mkabaji.



Msimu uliopita ulikuwa mzuri kwa Wanyama hadi kufikia baadhi ya timu ikiwemo Manchester United kumuweka kwenye listi ya wachezaji inayowawania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic