September 5, 2015


Na Haji Manara
Kitaaluma mm si kocha ingawa nilibahatika kupata mafunzo ya awali ya ukocha wa kandanda ambayo hainiongezei lolote kwenye taaluma hyo nzito.


Nimeangalia vizuri game yetu tena kwa jicho maalum la fikra chanya. Kwanza niwapongeze sana wachezaji wetu kwa kiwango chao, wamejitahidi sana. Nasema kiwango chao kwa sababu kisoka Nigeria ni mbingu na ardhi na sisi.

Bofu na pofu!
Mbuzi na swala!!
Kimsingi wamejituma sana leo na ndio silaha yao, ushindi wa sare leo ni kutokana na kujituma kuliko pitiliza toka kwa wapiganaji wetu wa Stars.

Yaan kujituma kwa Stars leo ukichanganya na uwezo wa Mbwana Samatta uwanjani kulikuwa zaid ya burudani pale Uwanja wa Taifa.

Kwangu Samatta ni mchezaji bora sana ambaye siamini bado analikata pori la  DR Congo hata kama tajiri Moise Katumbi anaendelea kumwaga faranga kwake.

Tuna uhaba mkubwa wa wachezaji wenye maamuzi bnafsi (si vipaji), bnafsi ni maamuzi ya kufanya jambo kwa ajili ya timu.
Kuamua kuchukua kijiji na kukisongesha mbele ni Samatta tu Tanzania kwa sasa!!

Ulimwengu pia ni mfano wa maamuzi hayo ingawa huathiriwa na uwezo wakati mwingine!
  
Ukijumlisha na kikosi chenye, ngoja nidadavue maksi kwa mtazamo wangu kabla sijaja kwa wakubwa wa mpira.


Ally mustafa710
Utulivu ni silaha ya golikipa huyu mpole na mchamungu

Shomari kapombe510
Kapombe bado hajarudi kwenye ubora wake kabla hajaenda Ufaransa. Anafanya makosa mengi na amepoteza kujiamini kwake

Haji Mwinyi710
Wajina wangu aliniangusha first half.ila kipindi cha pili baada ya Sunday Oliseh kubadilisha mfumo alisaidia sana kusuma mashambulizi.ingawa yupo dhaifu kwenye marking ya man to man


Nadir Haroub 'Cannavaro' 810
Kwangu legend huyu wa Yanga ni kisiki kamilii. Mipira yote ya juu alwayz ni chakula chake, ingawa speed yake imepungua mno. Lakini kwa mabeki tulionao, yeye bado anastahili kuendelea kuwa libero wa nchi

Kelvin yondani510
Uwepo wa Cannavaro na kutokuwa sharp kwa washambulizi wa kipopo ndio salama yake na yetu.
Mipira yote ya one against one kaachwa.
Rafu zisizo na tija.shukran refa kwa kumlinda stoper huyu.

Himid Mao mkami610
Neno pekee nnaloweza kusema kuhusu mido huyu ni mkabaji eneo sahihi wakati wote. Ila kwenye passes kaniangusha, kwani si ndefu wala fupi ingawa bado umri mdogo unamlinda.

Farid Mussa810
Nilianza kumfaidi kwenye Kagame, ni tunda linalosubiri kuliwa na taifa hili. Speed na ball control yake utaipenda, nna hakika akipata uzoefu tutakuwa na mchezaji wa level ya juu ingawa second half alikuwa taaaban.

Mrisho ngasa710
Anko anaweza asikupe maamuzi sahihi unapomtizamia ila kwa aina ya mifumo yetu na style yake anastahili kuendelea kutupa mbio zake ila yeye ndio aliokosa bao  la wazi zaidi na pia anko always huchelewa kutoa pasi wakati mwafaka.

Thomas Ulimwengu 910
Ni bull wa nchi kama tungekuwa na timu iliokamilika huyu ni old school striker ni kama gard muller au JJ Masiga.
Hebu pakini mabegi yenu kule Lubumbashi

Mudathir Yahya 710
Dynamo midfielder, msumbufu ingawa hukosa utulivu kwenye passes, ila ni mkabaji hasa na aliwachosha viungo wa Nigeria kwa tackling zake.

Mbwana Samatta 1010
Ningekuwa nacheza leo mpira ningependa kucheza na huyu pele wa nchi kwa sasa .
Vyovyote usemavyo ndio nyota wa mechi ya leo.

SUB
Said Ndemla 910
 Kwangu mimi sina la kusema kuhusu Ndemla ni samli kwenye mkate wa kusukuma. Ni computer wa kizazi cha sasa.
Akiongeza nguvu nnamuona angani kwenda kusukuma soka nje



Simon Msuva 610
Hakupata muda mrefu wa kucheza.ingawa pia hakuwa mbaya lakini bad luck, dogo papara zinakuwa zinamharibia.

John bocco 710
Ni mchezaji halisi wa kizazi hiki cha timu ya taifa.
Sijawahi kumuelewa ingawa inaonekana anapenda taifa lake.

Na lazma niwe mkweli umbile lake refu kwa mabeki ni hofu kwao na leo aliingia kipindi ambacho Ndemla alikuwa anadarsisha na yeye kung`ara pia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic