October 3, 2015

DULLY SYKES

Na Saleh Ally
Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Dully Sykes amesema anaamini adhabu aliyopewa beki Juma Nyosso ya kutocheza miaka miwili ni uonevu.


Dully ambaye anajulikana na nyimbo zake kama ‘Salome’, Julietha', 'Handsome', 'Bijou', 'Tamika' na ‘Ladie Free’ alizotamba nazo enzi zake, amesema Nyosso amekosea, hasa kurudia mara ya pili, lakini adhabu hiyo imekwenda kisiasa na kulenga kumkomoa.

“Sikiliza ndugu, mnapopambana kila mchezaji anafanya ujanja kuwachanganya wapinzani. Ikiwezekana anataka kumtengenezea kadi nyekundu mchezaji wa timu pinzani.


“Si umeona Chelsea kuna kila Diego Costa. Italia Mario Balotelli, pia unamkubuka Gazza wa England? Wote hao ni vichaa wa soka.

“Hata katika muziki tuna akina Balotelli, mafano mimi hapa. Pia kuna wachezaji wapole na wasanii wastaarabu kama akina AY, MwanaFA. Yote haya yapo.

“Nafikiri kama ni adhabu kutokana na makosa yake, basi wangempa adhabu ya miezi sita angalau, lakini sio miezi sita.

“Unajua wanataka kufanya hiyo kupiga (…..) ni kama kitu cha ajabu sana katika soka. Wakati ni mambo yanaendelea kila siku.

“Mimi nilikuwa kipa wakati nacheza soka, Nyosso ni beki wangu, nimekua naye pamoja kule Ilala. Hakuwa mtu wa namna hiyo, lakini najua alikuwa anapambana kwa ajili ya timu yake,” alisema Dully.

Tayari Nyosso ameanza kutumikia adhabu hiyo ikiwa ni ya pili baada ya ile kufungiwa mechi nane baada ya kumtomasa Elius Maguli wakati akiwa Simba, Januari mwaka huu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic