October 14, 2015


Kiungo mshambuliaji wa Azam FC, Khamis Mcha, amerejea rasmi uwanjani kuvaana na Yanga baada ya kuwa nje kwa miezi kadhaa huku kiungo Michael Bolou, akitarajiwa kuanza mazoezi mepesi wiki mbili zijazo.


Kiungo huyo ambaye pia anakipiga anakipiga katika timu yake ya taifa ya Zanzibar, alipata majeraha ya mguu hata kabla ya michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika mapema mwezi Julai mpaka Agosti, mwaka huu, baada ya kuvunjika mguu.

Daktari wa timu hiyo, Twalibu Misuli, alisema kwa wachezaji waliopo kambini kwa sasa, wote wapo fiti hata Mcha ambaye alikuwa nje, bado kidogo tu Bolou ambaye kwa sasa hawezi kucheza.

“Mcha kwa sasa yupo fiti, anaendelea na mazoezi na timu kama kawaida, hata katika mchezo wa Yanga ni jukumu la kocha kuweza kumtumia au kutomtumia lakini kiafya yupo vizuri kabisa.


“Lakini Bolou anatarajiwa kuanza mazoezi mepesi wiki mbili zijazo baada ya kumaliza programu maalum ambayo alipewa ndani ya mwezi mmoja, hivyo kwa sasa hakuna majeruhi wengine, zaidi tutawaangalia afya zao hao ambao wanatoka timu ya taifa,” alisema Misuli.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic