October 1, 2015

MASHABIKI WA MBEYA CITY
Uongozi wa Mbeya City, umeamua kuunda kamati maalum kuchunguza suala la beki na nahodha wake, Juma Said Nyosso.


Uamuzi huo umetokana na Nyosso kubainika akimtendea udhalilishaji nahodha wa Azam FC, John Bocco.

Taarifa zimeeleza, kamati hiyo itatoa majibu kesho kwa bodi ya jiji la Mbeya na baada ya hapo utaelezwa uamuzi hasa ni upi.

Tayari TFF imetoa adhabu kali ya miaka miwili kutocheza soka na faini ya Sh milioni mbili kwa Nyosso.

Lakini ajabu, pamoja na kuonekana kwenye picha akifanya jambo hilo, Nyosso ameanzisha kampeni za kukana jambo hilo.


Nyosso amekuwa akidai hakumbuki kufanya hivyo tena akinadai teknolojia inaweza ikawa inamhukumu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic