October 28, 2015




Straika hatari wa Taifa Stars, Mbwana Samatta anayekipiga katika timu ya TP Mazembe ya DR Congo ameahidi kufa na Algeria kwa kuisaidia timu yake kufanya vizuri licha ya kukiri kuwa mchezo utakuwa mgumu.


Stars inatarajia kukutana na Algeria  Novemba 14, baada ya kuiondoa Malawi katika mchezo wa kuwania kufuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia zinazotarajiwa kufanyika mwaka 2018 nchini Urusi huku mchezo wa marudiano ukichezwa Novemba 17.

Samatta akiwa Congo amesema kuwa, wanatarajia kukutana na upinzani mkubwa katika mchezo huo hasa ukizingatia wapinzani wao wapo vizuri na kudai kuwa yeye kama mchezaji wa kimataifa amejipanga ipasavyo kukabiliana na wapinzani wao  ili Stars iweze kusonga Mbele.

“Kwa upande wangu nimejipanga vizuri kuhakikisha timu yangu inasonga mbele na kutoa mchango wangu mkubwa katika hii mechi na nina mengi nitakayowashauri wezangu ili tuweze kushinda.

“Mechi itakuwa ngumu kwa upande wetu, ukiangalia Algeria walivyo kwa sasa na timu yao inavyoundwa na wachezaji wengi wenye viwango vizuri ni wazi mechi itakuwa na ushindani mkubwa.


“Kitu cha msingi tunachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha tunajipanga ili kuleta ushindani na kuweza kufanikiwa kufanya vizuri katika mchezo huo kwa kujituma na kutokata tamaa,” alisema Samatta.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic