November 4, 2015


Beki mkongwe wa Majimaji FC ya Songea, Fredi Mbuna, amefunguka kuwa licha ya kupokea kipigo cha mabao 6-1 dhidi ya Simba, kamwe hawawezi kushuka daraja kutokana na kipigo hicho.

Nahodha huyo wa zamani wa Yanga na sasa Majimaji, ni miongoni mwa wachezaji walioipandisha timu hiyo katika Ligi Kuu Bara na ameyaeleza hayo kutokana na kichapo kilichoanza kuzua hofu klabuni hapo.

Mbuna alisema kuwa kupoteza mchezo huo siyo sababu itakayowafanya washuke daraja.
“Kiukweli tumepoteza kwa idadi kubwa ya mabao, hatukutarajia kufungwa kwa idadi ile lakini haimaanishi kuwa sasa tutashuka.

“Sasa tutakachofanya ni kujituma zaidi ili tuweze kufanya vizuri kwenye michezo inayokuja huko mbele,” alisema Mbuna.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic