November 30, 2015





Na Saleh Ally
SEHEMU ya tatu nilieleza kuelezea namna ambavyo kulikuwa na baadhi ya mkanganyiko kati ya kamati ya Taifa Stars na baadhi ya viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wakati wa maandalizi ya mechi ya Taifa Stars dhidi ya Algeria.

Mfano lile la ndege ya Fastjet na TFF ikaamua kukata tiketi za gharama zaidi huku ikijua pamoja na gharama kuwa juu, timu ingeondoka bila mashabiki na hata waandishi wa habari ambao wangekosa unafuu wa safari hiyo.

Hiyo ilikuwa ni sehemu tu, lakini nakumbushia namna ambavyo niligundua watu walio nje wanavyotazama Taifa Stars tofauti na wengi walio ndani wanavyoliangalia suala hilo kwa maslahi zaidi.

Inapofikia mechi ya Taifa Stars, wengi wanakuwa wanafaidika kama mradi. Wanajua suala la tiketi lazima kutakuwa na kamisheni, suala la hoteli lazima watapata chao.

Hivyo mechi moja ya Taifa Stars, inaweza kuwafaidisha watu wengi sana ambao sit u watakuwa wanaifurahia mechi hiyo kama sehemu ya mafanikio au mapambano kwa ajili ya taifa letu. Badala yake ni kwa ajili ya faida yao na matumbo yao.

Vitengo vingi vya utendaji vya TFF, si vile ambavyo watendaji wake ni watu hasa wenye uwezo wa kusukuma gurumu la maendeleo. Ni watu ambao wako pale kutokana na utiifu wao kwa uongozi wa Jamal Malinzi.

Hiki ndicho ninachokiona si sahihi zaidi, ambavyo nilipiga kelele sana kuhusiana na mshauri wa ufundi wa Rais wa TFF, mtu mmoja hivi aitwaye Bwana Rutta.
Hana vigezo; hawezi kuwa mshauri wakati yeye anaamini ana uwezo tu wa fitina. Si mjuzi wa soka, hajawahi kuwa kocha, hajawahi kufundisha hata timu ya ligi kuu. Sasa anamshauri nini rais wa TFF, haya ndiyo mambo ya kishkaji ninayoyazungumzia.

Safari bado si fupi au ndogo kama wengi mnavyoona, kuwa ndani, angalau nikasogea na kuona TFF wanavyotenda mambo yao kwangu imekuwa faraja kubwa. Sasa ninajua na nina uwezo wa kuelezea mengi niliyonayo kwa vitendo.

Ningeweza kwenda mbali zaidi, lakini wakati ninahitimisha mwisho wa makala haya Jumamosi nitatoa ushauri wangu.

Kingine ambacho ninaweza kukielezea angalau kwa ufupi ni namna ambavyo TFF iliamua kuruhusu lundo la viongozi wake kwa Algeria. Wengi hawakuwa na kazi muhimu za kufanya, sijui walijua Stars itatolewa, kila mtu akataka anaglau asafiri tu ili ‘kufaidi’ mara ya mwisho!
Fedha walizozitumia maofisa hao, angalau zingetumika katika masuala mengine ya maendeleo, hata kama ni kununua mipira tu ya watoto, vijana au kazi nyingine kwa ajili ya maendeleo ya soka nchini.

Mara kadhaa, nimesema kuhusiana na Bwana Matandika ambaye mimi bado huwa sielewi hasa, anafanya nini TFF, kwa nafasi ipi, kazi ipi? Je, inaruhusiwa kikatiba na nani anayemlipa pale?

Mara kadhaa, nimekuwa nikiuliza. Lakini naamini kabisa, siku itafika na TFF hili litawasumbua kwa kuwa ni jambo wanaolichukulia kwa mzaha, lakini fedha zinazotumika ni mali ya Watanzania kwa kuwa hata kama ni udhamini wa timu ya taifa basi ni timu ya Watanzania. Fedha zinapaswa kutumika kwa ajili ya timu na mandeleo ya soka na si kuwapoza washikaji.

Lazima tukubali, kama tumeamua kuendeleza soka, basi tuwe makini. Mshikaji ambaye uwezo wake ni mdogo akae kando. Mnakumbuka namna Serikali ya Jakaya Kikwete ilivyoyumbishwa na washikaji kabla hajaamua kuchenji gia. Haya ndiyo yanayoukuta TFF kwa sasa.
Sehemu yangu ya mwisho kabla ya kujumuisha Jumamosi ni kambi ya timu ya taifa ya Afrika Kusini ambako nilikaa kwa takribani wiki hivi Stars ikijiandaa kucheza na Algeria mechi ya kwanza Novemba 17 jijini Dar es Salaam.

Kambi hiyo ilikuwa katika hoteli nzuri na ya kisasa ya Holiday Inn. Hoteli haikuwa ya kifahari kupindukia, lakini ilifaa kwa kambi na ulinzi ulikuwa mkali. Si lahisi watu kupita kutokana na ulinzi huo.

Timu ililazimika kusafiri kwenda kufanya mazoezi takribani kilimita 10 na ushee, ambalo halikuwa jambo baya kwa kuwa barabara ni bora, usafiri wa uhakika pia.

Kocha Charles Boniface Mkwasa na benchi lake la ufundi akiwamo mshauri mkuu, Abdallah Kibadeni, msaidizi wake, Hemed Morocco, kocha wa makipa Manyika Peter walifanya kazi yao, hakika kwa juhudi kabisa.

Chakula maalumu cha Kitanzania kiliandaliwa kila siku mchana na usiku. Hakika Kamati ya Taifa Stars kwa kushirikiana na TFF. Katika hili ninawapongeza, hakukuwa na kasoro kwao.

Wakati TFF na kamati walikuwa wamejitahidi katika hili. Makocha walipambana vilivyo, wachezaji hawakuwa ni wale wenye malengo, waliojitambua au kujua kwa nini wako pale na nitaanza kwa kuwataka kwa majina na upuuzi waliokuwa wakiufanya.

ENDELEA KUSOMA SEHEMU YA TANO

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic