Na
Saleh Ally
JUZI
Jumatano, nilielezea kuhusiana na wale viongozi rundo wa TFF waliosafiri na
timu. Wengi hawakuwa nafaida yoyote ya safari hiyo badala yake walikwenda kama
sehemu ya kwenda tu kwa kuwa kuna fedha za kuwaruhusu kwenda.
Huenda
waliona kila kitu kinawezekana kwa kuwa kuna fedha za udhamini wa Kilimanjaro dola
milioni 2, kwa mwaka zinazotolewa kwa ajili ya kuidhamini Taifa Stars.
Waliona inawezekana kwa kuwa tayari kamati ilijitokeza na kupunguza gharama ya mambo mengi ikiwemo kambi. Hivyo fedha ambazo zingeweza kutumika katika mambo mengine muhimu, wao wakaona zinaweza kutumiwa na wao kufurahia na kwenda kufanya ‘shopping’ ambalo lilikuwa ni jambo linaloonyesha wengi si wazalendo, hawako kwa ajili ya timu na wanaangalia zaidi maisha yao.
Ningependa
kuzama zaidi hata aina ya mfumo wa utendaji wa TFF ambao unaonekana ni “one man
show”. Mtu mmoja au kikundi Fulani kimejichukulia nguvu na kuwa sasa kinafanya
kinachotaka hata kama watendaji au wahusika, hawana uwezo kitaalamu wala
uzoefu.
Tuachane
na TFF, huenda siku nyingine nikawa na nafasi ya kuzama zaidi kwa kina na
kufunua madudu rundo ambayo ninayajua. Vema Watanzania wakajua maana kuna watu
watano ambao uwezo wao ni ziro, lakini wanashikilia sehemu nyeti na kamwe kwa
utendaji wao ulivyo, hakuna nafasi ya maendeleo hata kama watakuzwa vijana
1000!
Acha
nitumbukie katika ile kambi ya Taifa Stars iliyokuwa pale Johannesburg nchini
Afrika Kusini. Nilisema kambi ilikuwa katika hoteli bora ingawa haikuwa ya
kifahari kupindukia. Lakini hakika wachezaji au benchi la ufundi, haliwezi kuwa
na lawama.
Niwapongeze
TFF na kamati kwa kambi hiyo. Lakini nikashangazwa kabisa na mienendo au maisha
ya wachezaji ambao hakika ninaweza kukueleza nao ni tatizo kubwa.
Ninataka
kubainisha matatizo haya, kama utakuwa una nafasi, hifadhi ili ujue tunakwama
sehemu nyingi sana.
Wachezaji
wengi wa Taifa Stars hawana nidhamu kabisa. Ninaposema hivyo, sina maana ile
nidhamu ya kusema “shikamoo” au kuweka mikono nyuma wanapokuwa wanazungumza na
mtu anayewazidi umri.
Nifafanue
kwa kusema wengi si wachezaji wanaojitambua, hawajui kwa nini wako TAifa Stars
na huenda hawajui kuwa timu hiyo ya taifa ni kubwa kuliko klabu wanazozichezea.
Wapo tu kwa kuwa wapo na inaonyesha wanaamini kuwepo kwao pale wanaamini
wanaisaidia TFF au wanawasaidia Watanzania.
Nilianza
kushangazwa na tabia ya kuona wachezaji wengine wakiwa katika basi, halafu
wengine wanasubiriwa hadi unapofikia muda wa kwenda mazoezini, wakati mwingine
basi linalazimika kusubiri kwa kipindi fulani, eti fulani hajashuka katika
basi.
Suala
la kuchelewa liliendelea kujitokeza kadi katika chakula. Wengine wamefika na
wengine wangefika nusu saa baadaye tena wakitembea kwa mwendo wa kujidai tu.
Jambo ambalo lilionekana hawakuwa wakielewa maana hasa ya timu.
Ukiachana
na hilo, niliona jambo jingine la ajabu kabisa! Nikalazimika kwenda kuzungumza
na Charles Boniface Mkwasa ambaye alikiri kwamba aliliona na amelimekea mara
kadhaa.
Wachezaji
kuwa busy na Whatsapp, Instagram na Facebook. Wachezaji wengi wa Taifa Stars
walikuwa si wachezaji wa soka, badala yake ni wacheza mitandao.
Wengi
wao walipoteza muda mwingi wakisoma mitandao hiyo maarufu ya kijamii, tena
wasivyo na haya hata kidogo walikaa kwenye korido ya hoteli hadi saa 7 usiku
eti “wanachati”.
Nilishangazwa
nilipowakuta Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na Ibrahim Ajibu wakiwa wametoa mito
chumbani mwao halafu wamelala pale korido kila mmoja karibu na chumbani kwake,
“wanachati”.
Wanafanya
hivyo wakiwa kifua wazi, wamevaa bukta tu. Ajabu wamesahau hiyo ni njia ya
wapangaji wengine kwenda kwenye vyumba vyao, hivyo lazima waombe wakunje miguu
au wawaruke ili kupita kwa kuwa pale walipolala, kichwa kinakuwa upande wa
ukuta mmoja, miguu ukuta mwingine. Wameziba kabisa njia.
Jiulize
TFF, kamati zimelipa fedha kwa ajili ya chumba chenye kitanda kizuri, mazingira
bora. Lakini mchezaji anatoka nje na kwenda kulala kwenye njia tena akitumia
mtu ambao baadaye ataurejesha kitandani na kulalia, huo ni uchafu na uswahili
wa kupindukia.
Wachezaji
haohao, ndio waliokuwa wakihadithiana kuhusiana na nidhamu ya juu ya Mbwana
Samatta na Thomas Ulimwengu! Unajua walikuwa wanasemaje?
ENDELEA
KUSOMA SEHEMU YA SITA
0 COMMENTS:
Post a Comment