November 11, 2015


Uongozi wa klabu ya Simba umewaambia ule wa Yanga kama unataka kumsajili beki wao, Ramadhan Kessy, basi waende mezani kwa ajili ya kujadiliana nao pamoja na kupanga dau la kumuuza mchezaji huyo ambaye amekuwa akihusishwa kutakiwa na timu hiyo pamoja na Azam.

Kessy ambaye amebakiza miezi sita ya kuitumikia timu hiyo ya Simba inayonolewa na Muingereza, Dylan Kerr, ambapo kwa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa(Fifa) zinamruhusu beki huyo kufanya mazungumzo na timu yoyote ile kwa ajili ya kujiunga nayo.

Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano cha timu hiyo, Haji Manara alisema kuwa kama Yanga wana nia ya dhati ya kutaka kumsajili beki huyo basi wafanye mpango wa kuonana na uongozi wa timu yao kwa ajili ya kuangalia namna gani wanaweza kumruhusu beki huyo kuhama ndani ya kikosi chao.

“Tunasikia tu kuwa wapinzani wetu, Yanga wapo katika mchakato wa kutaka kumsajili mlinzi wetu, Ramadhan Kessy jambo ambalo sisi hatuna taarifa nalo zozote lile kwani wao mpaka sasa hawajaleta barua rasmi ya kuthibitisha kuwa wana nia ya kumsajili beki huyo.


“Lakini kama itakuwa kweli wanamtaka Kessy basi tunawaambia waje kuonana na uongozi wetu na kuweka mjadala wa kuangalia tunaweza kumuuza mchezaji huyo kwa dau gani haswa na kama tukifikia makubaliano tutamruhusu aende kwani sisi hatuna utamaduni wa kumng’ang’ania mchezaji ila siyo kumfuata mchezaji huyo kimyakimya wakati wanajua bado ni mali yetu,”alisema Manara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic