November 10, 2015


Taifa Stars imepoteza mechi yake ya kirafiki ya mazoezi dhidi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 kwa kufungwa mabao 2-0.


Mechi hiyo imechezwa kwenye Uwanja wa Eldorado nje kidogo ya jiji la Johanesburg na muda mwingi vijana hao wanaofundishwa na Shau Bartlet aliyewahi kuchezea Charlton Athletic ya England na Bafana Bafana walitawala zaidi kipindi cha kwanza kwa kiasi kikubwa.


Baada ya mechi hiyo, Kocha Charles Boniface Mkwasa alisema wachezaji wake walicheza kwa tahadhari kubwa kwa hofu ya kuumia.

"Lakini kikubwa lilikuwa ni suala la mazoezi na kuangalia makosa ni nini na kipi cha kurekebisha," alisema Mkwasa.

Baada ya mechi hiyo, Stars imemaliza rasmi kambi yake ya hapa Afrika Kusini na kesho inaanza safari kurejea nyumbani.



Kikosi cha Kikosi kilikachoanza leo:

1.   Aishi Manula
2.   Shomari Kapombe
3.   Haji Mwinyi
4.   Nadir Haroub
5.   Kelvin Yondani
6.   Jonas Mkude/Himid Mao
7.   Simon Msuva
8.   Salum Abubabary/Frank Domayo
9.   John Bocco/Elius Maguri
10.Mrisho Ngassa/Malimi Busungu
11. Farid Mussa/Salum Telela





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic