December 1, 2015


Mshambuliaji Robert Lewandowski wa Bayern Munich amekabidhiwa tuzo nne za rekodi maarufu kama Guinness World Records.


Lewandowski amekabidhiwa tuzo hizo baada ya kufunga mabao matano ndani ya dakika 8 tu wakati Bayern ilipoitwanga Wolfsburg kwa mabao 5-1 katika mechi ya Bundesliga.

Mshambuliaji huyo raia wa Poland aliingia katika mechi hiyo akitokea benchi wakati huo timu yake ilikuwa nyuma kwa bao 1-0.

Katika tuzo hizo nne za rekodi, zilikuwa zinawakilisha vipengele hivi; kupiga hat-tick ya haraka zaidi, kufunga bao nne haraka zaidi, bao tano za muda mfupi na aliyeingia na kufunga mabao mengi.

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic