Simba imemsajili beki, Novat Lufungo wa African Sports ya Tanga ili kuongeza nguvu katika kikosi chake.
Taarifa zinaeleza beki
huyo wa kati tayari ameishatua mjini Zanzibar na kujiunga na wenzake.
“Kweli Simba imemsajili
beki huyo kwa kumpa mkataba wa miaka miwili, ameungana na wenzake Zanzibar na
ameanza mazoezi,” kilieleza chanzo.
Simba iko mjini
Zanzibar ambako imeweka kambi kujiandaa na Ligi Kuu Bara ambayo tayari imeanza.
Simba imecheza mechi 9
tayari, iko katika nafasi ya tatu baada ya kufikisha pointi 21.
0 COMMENTS:
Post a Comment