July 1, 2016


Tukio la shambulio la kigaidi kwenye Uwanja wa Ndege wa Ataturk mjini Istanbul, Uturuki limebadili mipango ya Yanga kwenda kuweka kambi nchini huko kubadilika na badala yake inajipanga kwenda Pemba.

Yanga ilikuwa Antalya, Uturuki ilipoweka kambi kujiandaa na michezo yake miwili ya Kombe la Shirikisho, ikaahidi kurejea Uturuki baada ya mechi dhidi ya TP Mazembe, Jumanne ya wiki hii lakini sasa imebadili uamuzi.

"Timu itaondoka kesho (leo) kuelekea Pemba kwa ajili ya kambi ya muda kujiandaa na mechi na Medeama ambayo ni muhimu kwetu kupata ushindi ili hesabu ziende sawa.

"Sisi tulichopanga ni kushinda michezo yote iliyobaki ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kupoteza michezo miwili dhidi ya MO Bejaia na Medeama.

"Maamuzi hayo ya kambi ya Pemba yametokana na tukio kubwa la kigaidi lililofanywa huko Uturuki, hivyo kiusalama tumeona ni vema tukabaki nchini," alisema mtoa taarifa wetu.


Alipotafutwa Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro kuzungumzia hilo alisema: "Kambi yetu tutaitangaza wakati wowote wapi tutakapokwenda, hivyo subirieni kwanza tutawajulisha.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic