August 12, 2016


Mshambuliaji nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amezidi kuonyesha ubunifu hats katika biashara yake ya hoteli.

Katika moja ya hoteli anazozimiliki hoteli ya Pestana CR7 iliyoko jijini Lisbon nchini Ureno kwa kuwa kila mteja anayeingia anakutana na maneno ya kuhamasisha.

Maneno hayo ni yake ya kuwahamasisha wateja katika masuala mbalimbali ya maisha, kama vile “unaweza, usiwe muoga na usikate tamaa”, na kadhalika.

Mfumo huo unaonekana kuwa mpya kwa aina ya ukaribishaji wa wateja wanaofika kwenye hoteli hiyo.


Ronaldo aliamua kuingia katika uwekezaji wa hoteli, jambo ambalo wengi wamemsifia kwani utakuwa mtaji wa maisha yake baada ya kustaafu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic