Simba imepata sare ya bao 1-1 dhidi ya URA ya Uganda ambayo imeendelea kuwa ngumu kila inapokutana na Simba.
Mechi hiyo ilipopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo.
URA ndiyo walikuwa wa kwanza kufunga katika dakika ya 19 kupitia Mkungwa Alikanah kabla ya Simba kusawazisha kupitia Jonas Mkude.
Soka lilikuwa la kuvutia na URA waliendelea kuonekana ni timu bora kabisa.
Mechi hiyo ilikuwa rasmi kwa ajili ya kumuaga nahodha wake, Mussa Hassan Mgosi ambaye amestaafu rasmi.
0 COMMENTS:
Post a Comment