November 4, 2016



Rais John Pombe Magufuli ameeleza wazi namna anavyokerwa na tabia za mashabiki kung’oa viti uwanjani wakati timu zao zinapocheza.

Magufuli amesema amekuwa akifuatilia michezo, lakini alikerwa kuona mashabiki waking’oa viti.

Mashabiki wa Simba waling’oa viti wakati timu yao ilipokuwa ikicheza na Yanga.

Magufuli ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ikulu Dar es Salaam ikiwa ni siku ya kuadhimisha kutimiza mwaka mmoja tokea aingie madarakani.

“Nafuatilia michezo, napenda. Lakini nilichukizwa kuona watu wanang’oa viti.

“Waziri alifanya kazi nzuri ya kuwafungia. Ni vizuri kabisa kwa kuwa hawa watu hawajui uwanja unaotengenezwa kwa gharama kubwa, wao wanang’oa viti.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic