March 3, 2017

Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, kesho Jumamosi tarehe 04 Machi, 2017, watatembelea Kituo cha vijana wanaopatiwa matibabu baada ya kuathirika na dawa za kulevya.
Kituo hicho kinachoitwa Sober House kipo Bagamoyo mkoani Pwani. Ni kituo maalumu kwa tiba ya vijana kinaendeshwa na kusimamiwa na Shirika la Life and Hope Rehabilitation Centre chini ya Mkurugenzi, Al-Karim Bhanji.
 

Ikiwa huko, vijana wa Serengeti Boys ambao kwa sasa wako kwenye kipindi cha mabadiliko ya katika sayansi ya mwili hivyo itakuwa somo kubwa kwao katika kujielimisha kuhusu mustakabali wa maisha yao.
 

Kwa upande wa TFF kuwapeleka vijana hao huko ni utekelezaji Kanuni ya 36 (7) ya Ligi Kuu ya Vodacom inayozungumza kukataa rushwa, madawa, ubaguzi, fujo, kamari na mambo mengine ya hatari kwa mchezo wa mpira wa miguu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic