July 1, 2017



Nyota wa Barcelona, Lionel Messi amefunga ndoa na mpenzi wake wa utotoni.

Antonella Roccuzzo sasa ni mtu na mzazi mwenzake na wamefunga ndoa kwao Rosario, Argentina usiku wa kuamkia leo.
Kiasi cha wageni 250 wakiwemo nyota kadhaa waliocheza Barcelona zamani kama Xavi, Carles Puyol, Cesc Fabregas na Samuel Eto'o walihudhuria.

Baadhi ya nyota wanaocheza sasa pia kama Luis Suarez, Jordi Alba, Sergio Busquets walikuwepo.

Wale anaocheza nao timu ya taifa kama Sergio Agüero, Ezequel Lavezzi, Javier Mascherano na Angel Di Maria anayekipiga PSG pia walialikwa.
















0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic