Mtangazaji za kituo cha redio cha EFM, Seith
Katende maarufu kama Bikira wa Kisukuma, amefariki dunia leo katika Hospitali
ya Taifa MuhimbiliKwa mujibu wa baadhi ya wafanyakazi wenzake ambao hawakutaka
kutajwa majina yao kwa vile siyo wasemaji, walisema marehemu alianza kuugua
kiasi cha mwezi mmoja uliopita na msiba uko nyumbani kwa baba yake mzazi huko
Changanyikeni.
Marehemu ambaye alikuwa akitangaza kipindi
cha Ubaoni, kinachorushwa na redio hiyo kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, saa kumi
jioni, alikuwa pia ni bloga maarufu katika mitandao ya kijamii.
0 COMMENTS:
Post a Comment