KUMBE KOCHA NJOMBE NI MJANJA, AMETUMIA MBINU HII KUIMALIZA SIMBA LEO
Wakati pambano la Ligi Kuu Bara likisubiriwa jioni ya leo kati ya Njombe Mji FC dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe, Kocha Msaidizi wa timu ya Njombe, Mrage Kabange, ameeleza mbinu alizoziandaa kupata matokeo.
Mrage ameeleza kuwa walilazimu kupeleka nusu kikosi mjini Shinyanga kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Stand United na kubakisha kingine mjini Njombe.
Kocha huyo amesema iliwabidi wafanye hivyo ili wapate nguvu ya kupambana na Simba kwenye ligi kutokana na hali ya kikosi chao kuwa mbaya kwasababu wako kwenye mazingira ya kushuka daraja.
Taarifa zinaeleza kuwa kikosi cha Njombe kilichopelekwa Shinyanga kilikuwa na wachezaji wengi wa akiba na waliosalia Njombe walikuwa ni wale wa kikosi cha kwanza.
Uamuzi huo ulifanywa ili kuipa timu nguvu ya kupigania alama tatu muhimu dhidi ya Simba ambayo imekosa ubingwa wa ligi kwa miaka mitano sasa.
Mechi hiyo inachezwa leo Uwanja wa Sabasaba kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni.
Lazima upigwe
ReplyDeletehata wangebaki wote,kama uwezo hawana,watakuwa wamejinyima fulsa ya kuona miti inavyorudi nyuma tu.
ReplyDeleteHahahhahahaha,,mgonjwa anatafuta pa kufia kwa kwel
DeleteNaona kwakweli kikosi cha mnyama kiko kamili. Tunangoja kuusikia mngurumo wake
ReplyDeleteKwa kweli ni kitamu washindwe wenyewe tu
ReplyDelete