MFARANSA WA SIMBA ALETA STRAIKA HUYU WA KIMATAIFA, KAJA KUCHUKUA NAFASI YA OKWI
Kocha Mfaransa wa Simba SC, Pierre Lechantre, inaelezwa kuwa ameutaka uongozi wa klabu ya Simba kumsajili straika mwingine wa kimataifa atayekuja kurithi mikoba ya Mganda, Emmanuel Okwi.
Lechantre amegusia usajili huo ili kukiboresha zaidi kikosi hicho haswa katika safu ya ushambuliaji.
Kauli ya Mfaransa huyo, imetoka akiwa ana takribani miezi mitatu tu tangu aanze kukinoa kikosi hicho cha wekundu wa Msimbazi akipokea mikono ya Joseph Omog.
Simba hivi sasa ipo Morogoro kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar, utakaopigwa kesho Jumatatu kwenye Uwanja wa Jamhuri.
Straika huyu yupi???? Muwe makini mnapoandika habari waandishi
ReplyDeleteStraika huyu? Mbona hujamtaja?
ReplyDeleteStraika huyu? Mbona hujamtaja?
ReplyDeleteUkiona hivyo ujuwe hakuna jipya.
ReplyDeleteStraika huyu,,,halafu hakuna kitu,kwani okwi anaenda wapi
ReplyDeleteStraika huyu,,,halafu hakuna kitu,kwani okwi anaenda wapi
ReplyDelete