April 22, 2018



Na George Mganga


Mchezo pekee wa Ligi Kuu Bara leo Jumapili umemalizika katika Uwanja wa Sokoine Mbeya baina ya Mbeya City dhidi ya Yanga kwa kwenda sare ya bao 1-1.

Walikuwa ni Yanga walioanza kupata bao la kwanza kupitia Rafael Daud mnamo dakika ya 57 baada ya kumalizia vema mpira wa adhabu na kuandika bao hilo.

Mbeya City walimka na kuanza kutafuta bao la kusawazisha, lakini walipatwa na pigo kwa beki wake, Ramadhani Malima kutolewa nje kwa kadi nyekundu na kubaki 10 Uwanjani.

Katika dakika ya 93 zikiwa zimeongezwa 6 mpira kumalizika, Mbeya City walipata bao la kusawazisha kupitia kwa Iddy Naddo aliyefunga kwa kichwa kufuatia krosi safi iliyopigwa upande wa kulia mwa Uwanja.

Matokeo hayo yanaifanya Yanga ijipatie alama moja pamoja na Mbeya City, ambapo sasa imefikisha alama 48 kwenye msimamo huku watani zake wa jadi Simba wakiwa na 59.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic