June 10, 2018


FULL TIME: GOR MAHIA 2-0 SIMBA SC

Dak ya 93+3, Bado matokeo ni 2-0
Dak ya 90 zikiwa zimeongezwa tatu, Kagere anatolewa Uwanjani, nafasi yake inachukuliwa na Omondi
Dak ya 88, Nyavu zimekuwa za Gor Mahia ngumu kutikiswa na Simba
Dak ya 87, Mpira unaelekea kumalizika, zimebaki dakika 3
Dak ya 86, Kona imepigwa, imeokolewa na mabeki wa Simba
Dak ya 85, Hatari langoni mwa Simba, Tuyisenge anakosa kufunga bao la tatu, kona
Dak ya 81, Dakika 9 zimesalia mpira kumalizika
Dak ya 79, Gor Mahia waanashindwa kupata bao la nne, ilikuwa ni kasheshe kwenye lango la Simba

Dak ya 76, Faulo inapigwa kuelekezwa lango la Gor Mahia, anapiga Kichuuuya, inaokolewa
Dak ya 73, Kocha Masoud Djuma kasimama muda wote akizidi kuwahimiza vijana wake wazidi kupambana
Dak ya 70, Simba wameanza mpira vizuri eneo la kati, wametengeza shambulizi zuri lakini mbele wanashindwa kutengeneza bao
Dak ya 67, Gor wanafanya mabadiliko, anatoka Mieno, anaingia Wafula
Dak ya 66, Gor Mahia wanazidi kuliandama lango la Simba, mabeki wanaokoa, Bukaba naapiga mbele

Dak ya 64, Hali bado ngumu kwa Simba, ndoto ya kucheza na Everton inakuwa matatani
Dak ya 62, Hatariiii, Gor wanakosa bao la pili, Manula anaokoa, mpira ni kona
Dak ya 60, Mohamed Hussein ameingia kuchukua nafasi ya Yusuph Mlipili
Dak ya 59, Kagere anawakosakosa Simba kwa mara ya pili, wakati huo Simba wanafanya mabadiliko
Dak ya 54, Goooooal!! Tuyisenge anaipatia Gor Mahi bao la pili, ni 2-0
Dak ya 53, Bado Gor Mahia wanamiliki mpira zaidi ya Simba
Dak ya 52, Faulo nyingine inapigwa, awamu hii nikuelekea Simba
Dak ya 51, Faulo inapigwa kuelekea Gor Mahia, anapiga Kichuya, anapiga huku inamfikia Nyoni lakini anatoa mpira nje
Dak ya 49, Mpira umetoka, unarushwa kuelekea Gor Mahia
Dak ya 48, Bado Simba wanahaha kutafuta bao la kusawazisha, Gor Mahia wapo vizuri kwenye nafasi ya ulizi
Dak ya 47, Faulo inapigwa kuelekea Simba

HALF TIME: GOR MAHIA 1-0 SIMBA SC

Dak ya 45, Mohamed Rashid anaotea
Dak ya 44, Bado matokeo ni 0-0
Dak ya 42, Simba wanarusha mpira baada ya Gor kutoa nje, amerusha Kapombe, Gor wanaokoa
Dak ya 40. Tuyisenge enapewa kadi ya njano baada ya kuleta mabishano na Mwamuzi
Dak ya 38, Nyoni anapiga shuti kuelekea mbele, beki Gor Mahia anaokoa, bado Simba inahaha kupandisha mashambulizi mbele

Dak ya 36, Faulo inapigwa kuelekea Simba, pigwaaa Manula anadaka
Dak ya 34, Erasto Nyoni anapewa kadi ya njano baada ya kumchezea rafu Tuyisenge
Dak ya 33, Faulo nyingine tena kuelekea Simba, bado Gor wapo mbele kwa bao 1
Dak ya 31, Kocha wa Simba, Masoud Djuma aanamlalamikia Mwamuzi, wanazungumza
Dak ya 30, Faulo inapigwa kuelekea Simba, mchezaji Gor Mahia amechezewa madhambi

Dak ya 28, Manula ameanguka chini, kagongana na beki wa Gor Mahia
Dak ya 26, Kagere ameotea, mpira unaelekezwa Gor Mahia
Dak ya 26, Simba wameanza kuamka kidogo, mashambulizi ya zamu kwa zamu yameanza kuonekana
Dak ya 25, Gor wanapiga shuti kali, Manula anadaka
Dak ya 24, Mpira umetoka, Kichuya anarusha kuelekea Gor
Dak ya 24, Offside kwa Simba, mpira unapigwa kuelekezwa langoni kwao

Dak ya 23, Gor wanaotea, mpira unaelekezwa langoni kwao
Dak ya 22, Faulo inapigwa kuelekea Gor Mahia, anapiga Bukaba
Dak ya 21, Kapombe na mpira kati ya Uwanja, anajaribu kumpasia Rashid Juma lakini anapoteza

Dak ya 20, Tayari mpira umeshaanza, pigwa mbele huku unamfikia kipa wa Gor
Dak ya 19, Kagere ameumia, anapatiwa matibabu, mpira umesimama
Dak ya 18, Bukaba sasa na mpira, anatanguliza mbele huku lakini anakosa mwenzake
Dak ya 17, Hatari pale, Simba wanakosa kuandika bao la kusawazisha kufuata mpira wa krosi safi kutoka kulia mwa Uwanja, kipa anadaka
Dak ya 16, Salamba anadondoshwa chini, ni faulo inapigwa kuelekea Gor
Dak ya 14, Gor bado wanaumilikia zaidi mpira, wanajaribu kutafuta bao la pili
Dak ya 11, Kagere anapiga shuti moja kali langoni mwa Simba lakini mpira unakwenda nje

Dak ya 10, Mkude katikati ya dimba akiangalia nani wa kumpatia, piga mbele huku lakini hakuna mtu Gor wanaokoa
Dak ya 9, Offside, Gor wanaotea, Manula anaenda kupiga mpira kwenda mbele
Dak ya 9, Mkude anacheza faulo, Gor Mahia wanacheza
Dak ya 8, Gor Mahia wameanza kwa kasi takribani dakika 8 za mwanzo, bado wa njaa ya kufunga
Dak ya 7, Gor Mahia wanaanza baada ya Goli Kiki, umeshatoa, Simba wanarusha

Dak ya 6, Simba wanapelekea mpira kati, wanaanza
Dak ya 5, Goooooal, Kagere anaifungia Gor Mahia bao la kwanza
Dak ya 4, Mpira umerushwa kuelekezwa lango la Gor Mahia
Dak ya 3, Kagere anakosa nafasi ya kutengeneza nafasi nzuri ya kufunga, mpira umetoka
Dak ya 3, Faulo inapigwa kuelekea Simba, kushoto wa Uwanja
Dak ya 2, Mpira umeshaanza kutoka Uwanja wa Afraha, mjini Nakuru Kenya. Fainali ya SportPesa Super Cup

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic