July 26, 2018


Uongozi wa Klabu ya Azam, umeweka wazi kuwa msafara wa timu hiyo sambamba na benchi lake la ufundi utaondoka nchini Julai 30 kwa ajili ya kuelekea nchini Uganda watakapoenda ku­weka kambi ya muda mfupi ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi huku wakiondoka na wache­zaji wote katika msafara huo.

Azam FC chini ya kocha wake Hans van Der Pluijm itakuwa timu ya pili kwa msimu huu kutimkia nje ya nchi baada ya hivi karibuni Simba kukim­bilia Uturuki. Wanalambalamba hao wataenda Uganda kwa ajili ya kambi hiyo ambapo pia watakuwa na mich­ezo ya kirafiki.

Kwa mujibu wa Championi Juma­tano, Ofisa Habari wa Azam, Jaffar Idd amesema kuwa wataenda nchini humo Julai 30 wakiwa na kikosi kama ambavyo benchi la ufundi limependekeza kwa ajili ya kwenda kuwaona wachezaji wao vizuri na kutengeneza mipango ya msimu ujao.

“Tunatarajia kuondoka Julai 30 kwenda Uganda kama ambavyo tulipanga awali ambapo tukiwa huko tutakuwa na michezo ya kirafiki na wenyeji wetu wakiwemo Vipers ambao wamethibitisha kucheza na sisi kwa ajili ya ku­jipima nguvu.

“Tutaenda tukiwa na kikosi chetu kamili kama wataachwa wachezaji basi watakuwa wach­ache na kwa sababu maalumu lakini tofauti na hivyo hatutaweza kumuacha mchezaji yeyote yule kwa sababu kocha wamepend­ekeza twende na wachezaji wote,” alisema Idd.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic